Mara nyingi mastaa mbalimbali wamekuwa wakiishi maisha ya kuwafanya waonekana vyema mbele ya mashabiki wao na hata wengine kuishi maisha ambayo si yao ili mradi wawe kivutio kwa mashabiki wao.
Hilo limekuwa tofauti kidogo kwa mkongwe wa soka duniani David Beckham ambaye pia ni mwanamitindo baada ya kusema amekuwa akimtegemea mke wake Victoria kwa asilimia tisini na tisa katika uvaaji wake.
Beckam ambaye ni baba wa watoto watatu pia amesema yeye mara zote amekua akivutiwa na uhalisia wa maisha ya watoto wake ambao wamekuwa wakimvutia kwa kiasi kikubwa.
Mbali na Brooklyn amesema pia watoto wake wengine Romeo pamoja na Cruz nao wamekuwa wakimvutia wakati wote.
0 comments:
Post a Comment